Search This Blog

NATAKA ZOTE

 



NATAKA ZOTE

BY GIFT KIPAPA


Matone ya mvua yalidondokea kwenye kioo cha gari, huku kifaa cha kufuta maji kwenye kioo hicho

kikipita kusafisha, maji kutoka katika mitaro iliyofurika yalikuwa yakipita kukatisha bara bara, wakati foleni kubwa, iliyokuwa na magari yaliyoshonana hovyo sababu madereva wengine wamechepuka hadi pembezoni mwa bara bara kutafuta upenyo wa kupita, foleni hiyo haikuwa na hata dalili ya kusogea mbele.

Watu kibao walikuwa wakipita pembezoni mwa vibaraza vya maghorofa yaliyokuwa kando ya bara bara , ili kujikinga na mvua hiyo iliyokuwa inanyesha mfululizo.

Baadhi yao tayari walikuwa wamelowa na wengine wachache waliokumbuka kutembea na miamvuli walikuwa wakipita pembezoni mwa bara bara bila wasi wasi .

Wauza miamvuli walikuwa wakipiga kelele kupita jirani na watu waliokuwa wamejibaza kwenye maghorofa hayo wakinadi miamvuli yao, kuna walioshindwa kuvumilia na kununua miamvuli hiyo na wengine walijikausha kimya.

“hii sasa imezidi Roy, ukifanikiwa kutoka kwenye hii foleni , unajua mahali pa kunipata.”

Aliongea mrembo mmoja mwenye asili ya kizungu aliyekuwa ndani ya moja yua magari yaliyokuwa yamenasa kwenye msululu huo.

“ndio bibie.”

Aliitikia mwanaume aliyekuwa mbele ya gari hilo akiwa ameshikilia uskani.

Na halafu mrembo huyo alifungua mlango wa gari, matone kadhaa ya mvua iliyokuwa inanyesha kiupande upande yalimdondokea haraka haraka mwilini, lakini wala hakujali alitoka nje ya gari hilo na kisha kusimama kuangalia juu vile mvua ilivyokuwa inadondoka, kasi ya mvua iliongezeka na kufanya kitopu chake pamoja na suruali yenye kitambaa laini cha kubana vilowe.

“bibie, mwamvuli.”

Aliongea roy mara baada ya kufungua dirisha la gari na kumnyooshea bosi wake mwamvuli aliokuwa ameushikilia mkononi.

“ahsante, ila hapana Roy, wakati mwingine ni raha kunyeshewa na mvua.”

Aliongea huku akitabasamu na kuzitikisa tikisa nywele zake, na kuzifanya zirushe rushe maji, hakuwa yeye peke yake alienyeshewa na mvua hiyo japo wengine walionekana kukimbia wakitafuta sehemu ya kujibanza.

Alipita kati kati ya magari hayo huku mvua ikiendelea kumnyeshea, nguo zake zote zilikuwa zimeshikana na mwili wake kinoma na kuyafanya maungo yake yajichore ile ile.

Matiti yake yalikuwa yamejaa jaa hivi yalikuwa yakitikisika tikisika huku chuchu zake zikiwa zimechomoza hivi kwenye kitopu chake mvua nayo na vile kitopu hicho kilivyokuwa kimelowa basi kilikuwa kinaangaza matiti hayo kiasi kwamba mtu akiangalia anaweza sema hakuna kitu alicho vaa.

Chini nako suruali yani hadi mistari ya upinde wa chupi ilikuwa inaonekana na vile alivyokuwa anatembea kwa madaha basi alilifanya tako lake lililoshikwa na nguo kisawa sawa litikisike kwa staili Fulani iliyokuwa inatia nyege kinoma, wanaume waliokuwa kwenye magari hayo aliyoyapita walitoa macho kwa uchu ile kisenge.

Aliyapita magari hayo na kuchepuka kwa pembeni kwenye kijinjia kilichochongwa kando ya bara bara mara baada ya kuvuka mtaro wa maji akawa anatembea kwa kuruka ruka madimbwi ya maji yaliyokuwa kwenye kibara bara hicho.

“oya mtasha boda boda hapaaa.”

Aliongea mwanaume mmoja aliyekuwa anaendesha piki piki huku akiwa amevalia koti la mvua.

“unataka nipande boda boda yako?”

aliuliza mtasha huyo,

“ndio , ndio, nataka sana , ndio maana nipo bara barani na mvua hii , sababu ya pesa.”

Aliongea dereva huyo wa boda.

“sawa, nitapanda ila kwa sharti moja.”

Aliongea mzungu.

“sharti lolote nipo tayari, mradi utanilipa pesa tu.”

Aliongea mwanaume huyo.

“lolote?”

Aliuliza mzungu.

“lolote .”

Alisisitiza.

“nataka uvue hilo koti lako la mvua , tulowe wote njia nzima.”

Aliongea mzungu kauli iliyomfanya dereva huyo wa boda boda akae kimya kwa sekunde kadhaa.

“vipi mbona kimya hilo halikuwepo kichwani kwako wakati unasema upo tayari kwa lolote?”

Aliuliza mzungu.

“hapana lilikuwepo, lakini hilo linawezekana endapo utakuwa tayari kunikumbatia njia nzima.”

Aliongea dereva huyo, huku akiyaangalia matiti ya mzungu vile yalivyokuwa yamesimama alivuta hisia kichwani kwake vile atakavyojisikia endapo chuchu za matiti hayo zitaugusa gusa mgongo wake na kuutekenya tekenya akiwa amemkumbatia.

0 comments:

Post a Comment

Blog